Vipi Muislamu Anaupokea Mwezi Wa Ramadhani?
كيف يستقبل المسلم شهر رمضان؟
قال الشيخ ابن باز رحمه الله-:
Amesema Sheikh Al-Imaam Ibn Baaz Allah Amrehemu:
“ولا أعلم شيئاً معيناً لاستقبال رمضان سوى أن يستقبله المسلم بالفرح والسرور والاغتباط وشكر الله أن بلغه رمضان، ووفقه فجعله من الأحياء الذين يتنافسون في صالح العمل، فإن بلوغ رمضان نعمة عظيمة من الله. ولهذا كان النبي -صلى الله عليه وسلم- يُبشر أصحابه بقدوم رمضان مبيناً فضائله وما أعد الله فيه للصائمين والقائمين من الثواب العظيم، ويشرع للمسلم استقبال هذا الشهر المبارك بالتوبة النصوح، والاستعداد لصيامه وقيامه بنية صالحة وعزيمة صادقة”.
مجموع فتاوى ومقالات متنوعة (١٥/ ٩).
“Wala Siijui Kitu Chochote (Ibada) Maalumu (Mahsusi) Ya Kuukaribisha Mwezi Wa Ramadhani, Isipokuwa Ni Kuukaribisha Mwezi Huo Muislamu Kwa Furaha, Shangwe Na Bashasha, Na Kumshukuru Allah Kwa Kumfikisha Ramadhani Na Kumpa Tawfiq (Kumuafikisha) Akamfanya Miongoni Mwa Walio Hai Wanaoshindana Katika Matendo Mema. Hakika Kuifikia Ramadhani Ni Neema Kubwa Kutoka Kwa Allah.
Na Kwa Sababu Hiyo, Ndio Maana Mtume ﷺ Alikuwa Akiwabashiria Maswahaba Zake Kwa Kuja Na Kufika Kwa Ramadhani, Hali Ya Kuelezea Fadhila Zake Na Yale Aliyoyaandaa Allah Ndani Yake Kwa Wanaofunga Na Wanaosimama (Kwa Ibada Ya Usiku, Tarawehe n.k) Miongoni Mwa Thawabu Kubwa (Wanazozipata).
Na Inafaa (Inatakikana) Kwa Muislamu Aukaribishe Mwezi Huu Uliobarikiwa Kwa Toba (Kutubia) Ya Kweli, Na Kujiandaa Kwa Kuufunga Kwake Na Kusimama Kwake (Kwa Ibada Za Usiku) Kwa Nia Iliyokuwa Njema Na Azma Ya Kweli (Ya Dhati).”
(Majmuu’ Fataawaa Wa Maqaalaat Mutanawwi‘ah, Juzuu 15, Uk. 9)
Maelezo Mafupi:
Mwezi Wa Ramadhani Ni Mwezi Uliobarikiwa. Lakini Haina Maana Kuwa Umebarikiwa Ndio Watu Wazushe Mambo Katika Kuupokea Kwake, Mfano Watu Wengine Ikifika Tarehe 29 Ya Shaaban Wanasema Ni MWIRISHO Au VUNJA JUNGU, Wanapika Na Kufanya Mambo Ya Maasi, Hili Jambo Halijathibiti Bali Ni Uzushi Huu.
Na Wengine Wanafanya Makongamano Yakuukaribisha Mwezi Wa Ramadhani Kwa Kuweka Jitimai Katika Miji Na Viwanjani, Wanakesha Huko Na Weka Za Watu, Yote Haya Ni Katika Bidaa Na Mambo Yasiokuwa Na Dalili Yoyote Ile.
La Wajibu Kwa Muislamu Ajiandae Kama Alivyosema Sheikh Al-Imaam Ibn Baaz, Huo Ndio Uwajibu Kwake, Baarakallaahu Fiykum.
Mwandishi: Ustadh Abul Abbaas Anuari bin Ismail Asshaafiy, Allah Amuhifadhi.
Mchapishaji: salafussaalih.net
Tarehe: 29 Sha’abaan 1447H ~ 17 February 2026M