Ufafanuzi Kuhusu Kufunga Siku Tisa Za Mwanzo Za Dhul-Hijjah

التحرير في صيام الأيام التسعة الأول من ذي الحجة:

أما التاسع منها وهو يوم عرفة فصيامه سنة مؤكدة بلا شك ولاريب.

Ama Siku Ya Tisa Katika Hizo (Masiku Kumi), Nayo Ni Siku Ya Arafa, Basi Kufunga Kwake Ni Sunnah Iliyokokotezwa (Iliotiliwa Mkazo Kuifunga Kwake) Bila Shaka Wala Wasiwasi Wowote Ule.

وأما أيام الإثنين والخميس فمعلوم مواظبة النبي صلى الله عليه وسلم على صيام الإثنين والخميس فصيامها في تسع ذي الحجة سنة وصيامها آكد وأفضل من صيامهما في بقية العام.

Na Ama Siku Za Jumatatu Na Alkhamisi, Basi Inajulikana Kuwa Mtume ﷺ Alikuwa Akidumu Katika Kuzifunga Jumatatu Na Alkhamisi. Hivyo Basi Kuzifunga Kwake Ndani Ya Siku Tisa (9) Za Dhul-Hijjah Ni Sunnah, Na Kuzifunga Kunasisitizwa Zaidi, Na Ni Bora Zaidi Kuliko Kufunga (Jumatatu Na Alkhamisi) Katika Masiku Mengine Ya Mwaka (Yasiokuwa Kumi 10 Ya Mwanzo Ya Dhul-Hijjah).

وأما بقية أيامها فلا أعلم حديثاً ثابتاً في صوم النبي صلى الله عليه وسلم لها لكن نص الفقهاء على تأكد استحباب صيامها لعموم حديث: ( ما من أيام العمل الصالح فيهن… ) الحديث.

Na Ama Masiku Mengine Yaliyobakia (Katika Masiku Yake), Basi Mimi Sijui Hadithi Yoyote Ile Iliyo Thabiti Kwamba Mtume ﷺ Alikuwa Akiyafunga (Hayo Masiku Yote). Lakini Mafuqahaa (Wanawachuoni) Wametaja Juu Ya Kutilia Msisitizo Kuwa Inapendekezwa Kuyafunga (Masiku Hayo Yote 9) Kwa Ujumla Wa Hadithi (Inayosema):

“Hakuna Masiku Ambayo Matendo Mema Ndani Yake Yanapendwa Zaidi.…”

ويتأكد هذا العموم بفهم الصحابة لعموم الحديث لجميع الأعمال الصالحة.

Na Maana Hii Ya Ujumla Inatiliwa Mkazo Na Inathibitishwa Pia Na Ufahamu Wa Maswahaba Kuhusu Ujumla Wa Hadithi Kwa Matendo Yote Mema (Yanaingia Hapo Ikiwemo Funga).

فالخير في صيامها ومن اختار لنفسه عدم صيامها فلا ينبغي أن يسعى لصد الناس عن صيامها.

Kwa Hivyo Basi Kheri Imo Katika Kuyafunga (Masiku Hayo Yote Tisa 9). Na Atakayechagua Kutoyafunga (Masiku Hayo 9) Kwa Nafsi Yake, Basi Haifai Kufanya Juhudi Na Bidii Kuwazuia Watu (Wengine) Kufunga Masiku Hayo Tisa (9).

كتبه الشيخ سليمان الرحيلي حفظه الله تعالى في صفحته على تويتر (X). 19/6/2023

Ufafanuzi Huu Ameuandika Sheikh Suleiman Arruhaily Allah Amhifadhi Katika Ukurasa Wake Wa (X) Ambayo Zamani Ikiitwa Twitter. (19/6/2023M)

 

Maelezo Mafupi:

 

Kwahio Inafaa Kuzifunga Hizi Siku Tisa 9 Zote Kuanzia Tarehe 01 Ya Dhul-Hijjah Mpaka Tarehe 9 Ya Dhul-Hijjah Ambayo Ni Arafa. Wala Sio Vibaya Wala Sio Haramu Wala Sio Bida’a Kama Wanavyodhania Baadhi Ya Watu.

 

Vilevile Inafaa Kwa Mtu Kutozifunga Zote Ikiwa Anafunga Baadhi Ya Siku Tu. Lakini Jitahidi Muislamu Kama Unaweza Zifunge Zote 9 Ni Kheri Kubwa Zaidi Na Kama Huwezi Japo Jumatatu Zake Na Alkhamisi Zake Usiwache Kuzifunga, Na Pia Ukishindwa Kabisa Basi Usiwache Angalau Kufunga Siku Ya Arafa Ambayo Ndio Siku Ya Tisa 9 Yenyewe.

 

Mwandishi: Ustadh Abul Abbaas Anuari Bin Ismail Asshaafiy, Allah Amuhifadhi.

Mchapishaji: Salafussaalih.Net

Tarehe: 03 Dhul-Hijjah 1447H ~ 20 May 2026M