4. Neema Ya Amani
الأمن من أعظم النعم التي لا يستغني عنها الفرد ولا المجتمع.
AMANI Ni Miongoni Mwa Neema Kubwa Zaidi Ambayo Hawezi Mtu Kutosheka Nayo Mmoja Mmoja Wala Jamii Kiujumla. (Kila Mmoja Ni Mwenye Kuhitajia Hio AMANI).
Amesema Mtume ﷺ :
{مَنْ أَصْبَحَ مِنْكُمْ آمِنًا فِي سِرْبِهِ،
Yeyote Atakayeingia Asubuhi Miongoni Mwenu Hali Ni Mwenye AMANI Katika Nafsi Yake (Kizazi Chake, Familia, Jamaa Zake),
مُعَافًى فِي جَسَدِهِ،
Mwenye Siha Katika Mwili Wake,
عِنْدَهُ قُوتُ يَوْمِهِ، فَكَأَنَّمَا حِيزَتْ لَهُ الدُّنْيَا}
Ana Chakula Cha Siku Nzima , Basi Kana Kwamba Amekusanyiwa Dunia (Yote).
[رواه البخاري في “الأدب المفرد” والترمذي في “السنن”]
Hizi Ni Miongoni Mwa Neema Kubwa Kabisa Ambazo Anatakiwa Muislamu Azishukuru, Ikiwemo Hio Ya Kwanza Kabisa (AMANI). Kwahio Utajiri Sio Kuwa Na Majumba Na Magari Na Mapesa Mengi Tu, Bali Mwenye Vitu Hivyo Itakuwa Kana Kwamba Dunia Yote Amekusanyiwa Yeye.
Kwahio Muislamu Unataka Nini Tena Hapo Mpaka Ufanye Uharibifu Wa AMANI Ya Nchi Yako Kwa Kishingizio Tu Kuwa Eti Maisha Ni Magumu…!!! Una Maisha Magumu Gani?!! Na Neema Zote Hizo Upo Nazo Wewe Muislamu…!!!
Na Amesema Allah ﷻ Kuhusiana Na Neema Hii Ya AMANI Akiwakumbusha Mji Miongoni Mwa Miji Iliyopewa AMANI Na Utulivu Kisha Wakaikufuru Neema Hio Ya AMANI.
[وَضَرَبَ اللَّهُ مَثَلًا قَرْيَةً كَانَتْ آمِنَةً مُّطْمَئِنَّةً يَأْتِيهَا رِزْقُهَا رَغَدًا مِّن كُلِّ مَكَانٍ فَكَفَرَتْ بِأَنْعُمِ اللَّهِ فَأَذَاقَهَا اللَّهُ لِبَاسَ الْجُوعِ وَالْخَوْفِ بِمَا كَانُوا يَصْنَعُونَ] [النحل:112]
Na Allah Amepiga Mfano Wa Mji Ulio Kuwa Na AMANI Na Utulivu, Riziki Yake Ikiufikia Kwa Nafasi Kutoka Kila Mahali. Lakini Ukazikufuru Neema Za Allah, Kwa Hivyo Allah Akauvika Vazi La Njaa Na Khofu Kwa Sababu Ya Yale Waliyokuwa Wakiyafanya. [Surat an-Nahl:112]
قال الإمام السعدي رحمه الله:
Amesema Mwanawachuoni Al-Imamu Assa’adiy Allah Amrehemu:
وهذهِ القريةُ هي مكَّةُ المشرَّفةُ التي كانتْ آمنةً مطمئنةً.
“Na Huu Mji (Uliotajwa Katika Aya Hii) Ni Mji Wa Makka Mtukufu Ambao Ulikuwa Ni Wenye AMANI Na Utulivu.
فأذاقَهم اللُه ضِدَّ ما كانُوا فيهِ، وأَلْبَسَهم لِبَاسَ الجوعِ الذي هو ضِدُّ الرَّغَدِ، والخَوْفُ الذي هو ضدُّ الْأَمْنِ، وذلك بسبَبِ صَنِيعِهم وكفْرِهم وعدَمِ شُكْرِهم.
Basi Allah ﷻ Akawaonja Wao Kinyume Ya Vile Walivyokuwa Mwanzo (Ndani Yake) Kuwa Na AMANI Na Utulivu, Na Akawavika Vazi La Njaa Ambalo Ni Kinyume Cha Ukunjufu Wa Rizki, Na (Akawavika) Khofu Ambayo Ni Kinyume Cha AMANI, Na Hilo Nikutokana Na Sababu Ya Kitendo Chao Na Kufuru Yao (Ya Neema Hizi Ikiwemo AMANI Na Utulivu) Na Kutokushukuru Kwao (Neema Hio Ya AMANI Na Utulivu)”.
Kwahio Tumshukuru Allah Kwa Kutupa Neema Hii Ya AMANI Na Tusikubali Kushawishiwa Na Mtu Yeyote Yule Kuivunja AMANI Hii Kwa Kishingizio Tu Eti Maisha Ni Magumu, Na Mambo Mengine Ambayo Hayana Msingi Wowote Ule.
MWISHO.
Mwandishi: Ustadh Abul Abbaas Anuari Ismail Ali Al-Zinjibaary Asshaafi’y, Allah Amuhifadhi.
Mchapishaji: salafussaalih.net
Tarehe: 01 Jumaada al-Awwal 1447H