3. Neema Ya Amani
الأمن من أعظم النعم التي لا يستغني عنها الفرد ولا المجتمع.
Amani Ni Miongoni Mwa Neema Kubwa Zaidi Ambayo Hawezi Mtu Kutosheka Nayo Hio Amani Mtu Mmoja Mmoja Wala Jamii Kiujumla. (Kila Mmoja Ni Mwenye Kuhitajia Hio Amani).
Allah ﷻ Anaendelea Kuwakumbusha Maqureish Na Waislamu Kiujumla Kuhusiana Na Neema Hii Ya Amani Na Neema Ya Rizki Juu Yao Akasema:
[الَّذِي أَطْعَمَهُم مِّن جُوعٍ وَآمَنَهُم مِّنْ خَوْفٍ] [القريش: 4]
(Allah ﷻ) Ambaye Anawalisha (Kutokana) Wasipate Njaa, Na Anawalinda (Kuwaaminisha Kuwapa Amani) Kutokana Na Khofu. [Surat al-Quraysh:4]
قال الإمام السعدي رحمه الله:
فَرَغَدُ الرِّزْقِ وَالْأَمْنُ مِنَ الْمَخَاوِفِ، مِنْ أَكْبَرِ النِّعَمِ الدُّنِيَوِيَّةِ، الْمُوجِبَةِ لِشُكْرِ اللهِ تعالى. [تفسير السعدي]
Amesema Mwanawachuoni Al-Imamu Assa’adiy Allah Amrehemu:
Basi Wasaa (Ukunjufu) Wa Rizki (Uzuri Wa Rizki), Na Kupata Amani Kutokana Na Vitu Venye Kuogopesha (Mfano Mauaji n.k.), Ni Katika Neema Kubwa Zaidi Za Kiulimwengu (Zakidunia), Zenye Kuwajibisha (Kwa Neema Hizo) Kumshukuru Allah ﷻ. (Tafsiiru Assa’adiy)
Akaendelea Allah ﷻ Kuwakumbusha Tena Maqureish Kutokana Na Neema Hii Ya Amani Akasema:
[أَوَلَمْ يَرَوْاْ أَنَّا جَعَلْنَا حَرَمًا ءَامِنًا وَيُتَخَطَّفُ ٱلنَّاسُ مِنْ حَوْلِهِمْ ۚ أَفَبِٱلْبَٰطِلِ يُؤْمِنُونَ وَبِنِعْمَةِ ٱللَّهِ يَكْفُرُونَ] [العنكبوت: 67]
“Je! Hawaoni Ya Kwamba Tumeifanya Nchi Takatifu (Makka) Ina Amani, Na Hali Watu Wengine Wananyakuliwa Kote Kwa Majirani Zao? Je! Wanaamini Upotovu, Na Neema Za Allah Wanazikataa?” [Surat al-‘Ankabut:67]
Maelezo……
إنَّ اللهَ خصَّها بالذِّكْرِ دُونَ سائرِ الْبُلدانِ وهو ربُّ الْبِلَادِ كلِّها، لأنه أرادَ تعريفَ المشركينِ بنعمتِه عليهم وإحسانِه إليهم، وينبغِي أن يعبدُوهُ هو الذي حرَّمَ بَلَدَهم فمنعَ الناسَ منهم وهم في سائرِ البلادِ يأكلُ بعضُهم بعضاً ويَقْتُلُ بعضُهم بعضاً.
Hakika Ya Allah ﷻ Ameuhusisha Mji Wa (Makka) Kwa Kuutaja Pasina Na Kuitaja Miji Mengine, Na Hali Yakuwa Yeye Allah ﷻ Ni Mola Mlezi! Wa Miji Yote, Kwasababu Yeye Allah ﷻ Anataka Kuwafahamisha Washirikina Kwa Neema Yake Hio Ya (Amani) Juu Yao Na Kuwafanyia Wema Kwao (Hao Maqureish), Na Inatakikana Wamuabudu Yeye Allah ﷻ Yeye (Allah) Ndie Alieharamisha (Kuufanya Mtukufu Mji Wao Wa Makka) Akawazuiya Watu Wengine Kutokana Na (Kuwadhuru Wao) Na Hali Yakuwa Wao (Watu Wengine) Katika Miji Yao Mengine Wanakulana Wao Kwa Wao (Kudhuriana) Na Wanauwana Kwa Baadhi Ya Wengine Kuwauwa (Watu) Wengine (Wao Kwa Wao).
Itaendelea In Shaa Allah….
Mwandishi: Ustadh Abul Abbaas Anuari Ismail Ali Al-Zinjibaary Asshaafi’y, Allaah Amuhifadhi.
Mchapishaji: salafussaalih.net
Tarehe: 22 Rabiu al-Thaaniy 1447H