2. Neema Ya Amani

الأمن من أعظم النعم التي لا يستغني عنها الفرد ولا المجتمع.

 

AMANI Ni Miongoni Mwa Neema Kubwa Zaidi Ambayo Hawezi Mtu Kutosheka Nayo Hio Amani Mtu Mmoja Mmoja Wala Jamii Kiujumla. (Kila Mmoja Ni Mwenye Kuhitajia Hio Amani).

 

Kutokana Na Neema Hii Ya AMANI,

 

Ndio Maana Alikuwa Mtume Muhammad ﷺ Pindi Anapoona Mwezi Muandamo (Mwezi Unapoandama Na Kuingia Mwezi Mwengine) Akisema:

 

{الله أكبر اللهم أهلَّه علينا بالأمن والإيمان والسلامة والإسلام والتوفيق لما تحب وترضى ربنا وربك الله}

 

“Allah ﷻ Ni Mkubwa , Ewe Allah ﷻ Uanzishe Kwetu (Huo Mwezi) Kwa AMANI, Na Imani Na Usalama Na Uislamu, Na Taufiq Yakile Unachokipenda Mola Wetu Na Kukiridhia, Mola Wetu Na Wako Ni Allah ﷻ.”

 

Kuonesha Umuhimu Wake AMANI, Akiiomba Hio AMANI Kila Mwezi Unapoingia Ili Allah ﷻ Aidumishe AMANI Hio. Muislamu Anatakikana Kuihifadhi Neema Hii Ya AMANI Na Kuidumisha Kwenye Miji Na Kuishukuru Neema Hii.

 

Na Ibada Haziwezi Kufanyika Ukweli Wakufanyika Kwa Ibada Hizo Juu Ya Ukamilifu Wake Zaidi, Na Namna Yake Inavyotakikana Ispokuwa Ipatikane AMANI. Ndio Maana Allah Akasema:

 

[فَإِذَا اطْمَأْنَنتُمْ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ] [النساء:103]

 

Na Mtapo Tulia (Kutokana Na Khofu) (Mukapata AMANI) Basi Shikeni Sala Kama Dasturi (Ilivyo). [Surat an-Nisaa:103]

(Maana Yake Itekelezeni Hio Swala Kwa Ukamilifu Wake Na Namna Yake Iliyotimia Pindi Tu Itakapoondoka Khofu Hio Na Mukapata AMANI).

 

Kwahio Bila Ya AMANI Hawezi Muislamu Kutekeleza Ibada Yake Kwa Utulivu Na Huenda Hata Misikiti Ikafungwa Kwa Kuhofia Watu Nafsi Zao Kuuwawa Kwa Uvunjifu Wa AMANI.

 

DUMISHA AMANI EWE MUISLAMU USITOKE BARABARANI KWA  KUFANYA MAANDAMANO….!!!

 

Kwenye Uislamu Hakuna Kitu Kinachoitwa Maandamano Haya Yote Ni Mambo Ya Makafiri Achana Na Mila Zao Hizi Na Fuata Uislamu Wako, Kwa Kukaa Ndani Ya Nyumba Yako Wakati Wa Fitna Kama Hizi.

 

Itaendelea In Shaa Allah….

 

Mwandishi: Ustadh Abul Abbaas Anuari Ismail Ali Al-Zinjibaary Asshaafi’y, Allaah Amuhifadhi.

Mchapishaji: salafussaalih.net

Tarehe: 18 Rabiu al-Thaaniy 1447H