Ubora Wa Masiku Kumi Ya Mwanzo Ya Dhul Hijjah

Alhamdulillahi Waswalatu Wasalaaam Alaa Rasuulillah Wabaad:

قال الله تعالى:

وَٱلۡفَجۡرِ ١ وَلَيَالٍ عَشۡرٖ ٢

Amesema Allah Aliyetukuka:

Naapa Kwa Wakati Wa Alfajri. Na Ninaapa Kwa Masiku Kumi.

 

Mola Aliyetukuka Ni Mtukufu Haapi Ila Kwa Yale Yaliyo Matukufu. Hakuna Shaka Kuwa Haya Ni Masiku Bora Katika Masiku Ya Dunia. Kuyatumia Vema Masiku Haya Kwa Kutenda Amali Njema Zinazomridhisha Allah.

 

لقد ثبت الحديث الذي رواه البخاري والترمذي واللفظ له عن عبد الله ابن عباس رضي الله عنه قال : قال رسول الله صلى الله عليه وسلم ما من أيام العمل الصالح فيهن أحب إلى الله من هذه الأيام العشر قالوا : يا رسول الله ولا الجهاد في سبيل الله؟ فقال ولا الجهاد في سبيل الله إلا رجل خرج بنفسه وماله فلم يرجع من ذلك بشيئ

Imethibiti Hadithi Ambayo Ameipokea Imam Bukhari Na Tirmidhi Katika Sunan Zao, Na Tamko La Riwaya Hii Ni La Tirmidhi.

Kutoka Kwa Abdillahi Ibnu Abbass Allah Amridhie Amesema: Amesema Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake: Hakuna Katika Masiku Ambayo Matendo Yake Yanapendeza Mbele Ya Allah Kuliko Masiku Kumi Ya (Mwanzo Wa Dhulhija). Maswahaba Wakamuuliza Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake. Hata Jihadi Katika Njia Ya Allah? Rasul Akajibu: Hata Jihadi Katika Njia Ya Allah Ispokuwa Mtu Ambaye Ametoka Katika Njia Ya Allah Kwa Nafsi Yake Na Mali Yake Na Hakurejea Na Chochote.

Twajifunza Kuwa Matendo Mema Ndani Ya Mwezi Wa Dhulhijja Yanaziada Ya Malipo Zaidi.

 

Maneno Ya Mwandishi

Tukithirishe Kufanya Adhkari Na Bora Ya Adhkari Ni Kuisoma Qur an.

 

Tutoe Swadaka Kwa Kuwa Mwenye Kutoa Hupewa Badali.

 

Tuunge Udugu Kwa Sababu Ni Miongoni Mwa Mambo Yanayomfanya Mja Kukunjuliwa Rizki Zake.

 

Tutendeane Mema Bali Pia Kuamrishana Na Kukatazana Maovu.

 

Tunakuomba Mola Wetu Uliyetukuka Uturuzuku Matendo Yenye Kukubaliwa Na Dua Zenye Kujibiwa.

 

Rejea
1.Suratul Fajir 1Na 2

2.Sahihi Bukhar 969

3.Sahihi Tirmidh757

 

Mwandishi: Sheikh Abu Hanifa Salim Mwinyi, Allah Amuhifadhi.

Mchapishaji: salafussaalih.net

Tarehe: 01 Dhul-Hijjah 1447H ~ 18 May 2026M