Tanbihi Muhimu Kwa Yule Mwenye Kutaka Kuchinja Udh’Hiya

عن أم سلمة رضي الله عنها، أن النبي ﷺ قال: ” إذا رَأَيْتُمْ هِلالَ ذِي الحِجَّةِ، وأَرادَ أحَدُكُمْ أنْ يُضَحِّيَ، فَلْيُمْسِكْ عن شَعْرِهِ وأَظْفارِهِ “.

صحيح مسلم: (1977).

Kutoka Kwa Ummu Salamah Allah Amridhie: Hakika Mtume ﷺ Amesema: “Pindi Mutakapo Uona Mwezi Muondamo Wa Dhul-Hijjah (Mfunguo Tatu), Na Mmoja Wenu Akataka Kuchinja Udh’Hiya, Basi Ajizuilie (Aache Kukata) Nywele Zake Na Kucha Zake (Na Ngozi Yake Pia).”

Sahih Muslim (1977).

هذا الحديث خاص بمن أراد أن يضحي فقط، أما المُضحَّى عنه فسواء كان كبيرًا أو صغيرًا فلا مانع من أن يأخذ من شعره أو بشرته أو أظفاره بناءً على الأصل وهو الجواز.

فتاوى اللجنة الدائمة (١١ / ٤٢٦)

 

Hadithi Hii Ni Mahsusi (Ni Maalumu) Kwa Yule Mwenye Kutaka Kuchinja Udh’Hiya Tu Peke Yake. Ama Anayechinjiwa, Awe Mkubwa Au Mdogo, Hakuna Ubaya Kwake Kuchukua (Kwa Kukata) Katika Nywele Zake, Ngozi Yake Au Kucha Zake, Kwa Sababu Yakujengea Asili (Ya Jambo Hili) Nayo Ni “Jawazi” (Kufaa Kufanya Hivyo).

Fataawa Al-Lajnah Ad-Daaimah (11/426).

 

⁠ ⁠قال ابن قدامة رحمه الله: إذا ثبت هذا, فإنه يترك قطع الشعر وتقليم الأظفار, فإن فعل استغفر الله تعالى، ولا فدية فيه إجماعا, سواء فعله عمداً أو نسياناً.

المغني (٣٤٦/٩).

 

Amesema Al-Imaam Ibn Qudaamah Allah Amrehemu:

Likithibiti Hili (Lakutaka Kuchinja Udh’Hiya), Basi Huacha Yeye Kukata Nywele Na Kupunguza (Kukata) Kucha. Basi Akifanya Hivyo (Kukata Nywele, Kucha Na Ngozi Yake) Basi Amuombe Allah Msamaha, Wala Hana Fidia Kwa Makubaliano Ya Wanachuoni, Sawa Akiwa Amefanya Kwa Makusudi Au Kwa Kusahau.

Al-Mughniy (9/346).

 

 

Maelekezo Mafupi:

Haifai Kwa Yule Aliekusudia Kuchinja Udh’Hiya Kukata Nywele Zake, Kucha Zake Na Ngozi Yake. Na Hili Ni Haki Yake Yeye Tu, Ama Watu Wanyumbani Kwake Wao Wanaruhusiwa, Na Vile Vile Yule Aliewakilishwa Kuchinja Udh’Hiya, Na Mchinjaji Na Mwenye Kusimamia Haingii Kwenye Katazo Hili. Katazo Hili Ni Maalumu Kwa Yule Mwenyewe Aliekusudia Kuchinja Udh’Hiya Tu Peke Yake. Na Ngozi Inayokusudiwa Ni Ngozi Ya Mwili Ambayo Imezidi Au Imeharibika, Mfano Kwenye Kidonda n.k, Hatakiwi Kuikata Kwanza Mpaka Atakapochinja Udh’Hiya Yake.

 

Mwandishi: Ustadh Abul Abbaas Anuari bin Ismail Asshaafiy, Allah Amuhifadhi.

Mchapishaji: salafussaalih.net

Tarehe: 29 Dhul-Qaadah 1447H ~ 17 May 2026M