Hadithi Ya Leo: Hakuna Masiku Yaliyo Bora Zaidi Mbele Ya Allah Kuliko Masiku Kumi 10 Ya Dhul-Hijjah
عن جابر بن عبدالله رضي الله عنهما، أن رسول الله ﷺ قال: ” ما من أيامٍ أفضلُ عندَ اللهِ من أَيَّامِ عَشْرِ ذِي الحِجَّةِ “.
📚 صحيح الترغيب للألباني (١١٥٠)
Kutoka Kwa Jaabir Ibn Abdillaah Allah Amridhie: Kwamba Mtume ﷺ Amesema: “Hakuna Masiku Yaliyo Bora Zaidi Mbele Ya Allah Kuliko Masiku Kumi 10 Ya Dhul-Hijjah”.
قال العلامة ابن عثيمين رحمه الله: يظن بعض الناس أن العشر الأواخر من رمضان أفضل من العشر الأوائل من شهر ذي الحجة والأمر بالعكس؛ ربما يستغرب كثير من الناس هذا لجهله ولذلك تجد العشر الأوائل من شهر ذي الحجة تمر بالناس ولا يقدرون لها قدرها لا في الصيام ولا في الصدقة ولا في قراءة القرآن ولا بكثرة الصلاة، لأنهم يجهلونها
📚 فتاوى الحرم المكي
Amesema Sheikh Muhammad Ibn Salih al-Uthaymeen Allah Amrehemu:
“Baadhi Ya Watu Hudhania Kwamba Masiku Kumi 10 Ya Mwisho Ya Ramadhani Ni Bora Zaidi Kuliko Masiku Kumi 10 Ya Mwanzo Ya Dhul-Hijjah, Hali Ya Kuwa Jambo Ni Kinyume Chake (Masiku Kumi 10 Ya Dhul-Hijjah Ni Bora Zaidi Michana Yake). Huenda Watu Wengi Wakastaajabu Hili Kutokana Kwa Ujinga Wao (Wakutosoma Dini). Ndiyo Maana Unakuta (Unaona) Masiku Kumi Ya Mwanzo Ya Dhul-Hijjah Yanapita Kwa Watu Bila Kuyapa Hadhi Yake (Na Heshima Yake); Si Katika Kufunga (Hawafungi Saumu), Wala Sadaka, Wala Kusoma Qur’an, Wala Kuzidisha Swala, Kwa Sababu Hawajui Ubora Wake”.
Mwandishi: Ustadh Abul Abbaas Anuari bin Ismail Asshaafiy, Allah Amuhifadhi.
Mchapishaji: salafussaalih.net
Tarehe: 01 Dhul-Hijjah 1447H ~ 18 May 2026M