3. Fadhla Za Swahaba Abuubakr Radhi Za Allah Ziwe Juu Yake

Swahaba Huyu Jina Lake Ni Abdillaah Ibnu Uthmaan Ibnu Murrah Ibnu Kaab Ibnu Abiy Quhafah.

 

Abuubakr Alizaliwa Mwaka 573 Milaadiyyah Katika Mji Wa Makkah.

 

Abubakar Ni Mtu Wa Mwanzo Kusilimu Katika Wanaume Wa Makkah.

 

Ni Mtu Wa Mwanzo Kujitolea Kuihami Dini Na Kumuhami Mtume Katika Mazingira Magumu Mwanzoni Mwa Uislam.

 

Na Maswahaba Wengi Wamesilimu Chini Ya Abuubakr Swiddiiq.

 

Miongoni Mwa Watoto Wake Ni ‘Aaishah Bint Abiybakri Allah Amuwie Radhi.

 

Alimuozesha Mtume Bint Yake Kwa Mapenzi Makubwa Aliyonayo Juu Ya Mtume Wa Allah.

 

Ndiye Mtu Pekee Aliyeinunua Ardhi Kwa Ajili Ya Kujengwa Msikiti Mtakatifu Wa Madinah.

 

Katika Maneno Mazuri Aliyoyataja Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake Ni Kuwa:

 

Lau Imani Ya Abuubakri Itapimwa Katika Mizani Na Imani Za Watu Wengine Basi Imani Ya Abuubakri Itashinda.

 

Miongoni Mwa Ubora Wa Abuubakri Alikuwa Ni Mtu Mwema Na Mcha Mungu Sana.

 

Allah Ametaja Katika Qur’aan Katika Kumtakasa:

 

[وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى]

 

Na Ataepushwa Nao Huo Moto Aliyemcha Mungu Mno. [Suurat Al-Layl:17]

 

Alikuwa Mweledi Katika Mambo Ya Dini.

 

Alikuwa Ni Mwenye Kudumu Mnoo Katika Ibada Za Faradhi Pia Ibada Za Sunnah.

 

Imesimuliwa Hadith Ambayo Ameipokea Imam Muslim.

 

عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: من أصبح منكم اليوم صائما؟
قال أبو بكر: أنا.
فمن أتبع منكم اليوم جنازة؟
قال أبو بكر: أنا.
قال فمن أطعم منكم اليوم مسكينا؟
قال أبو بكر :أنا.
فمن عاد منكم اليوم مريضا؟
قال أبو بكر أنا.
قال رسول الله صلى الله عليه وسلم ما اجتمعن في امرئ إلا دخل الجنة.
رواه مسلم.

 

Kutoka Kwa Abu Hurayrah Radhi Za Allah Ziwe Juu Yake Kuwa Amesema: Amesema Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake Kuwaambia Maswahaba Ni Nani Miongoni Mwenu Ameamka Hali Ya Kuwa Amefunga…?

Abubakar Akajibu.

Mimi (Ewe Mtume Wa Allah).

Mtume Akauliza Ni Nani Miongoni Mwenu Leo Amesindikiza Jeneza?

Akasema Abuubakr Mimi.

Kisha Akauliza Tena Mtume Ni Nani Miongoni Mwenu Amelisha Maskini?

Abuubakr Akajibu Mimi.

Kisha Akauliza Ni Nani Miongoni Mwenu Leo Amemtembelea Mgonjwa?

Abuubakr Akajibu Mimi.

Akasema Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake, Hayakusanyiki Mambo Haya Kwa Mtu Ila Mtu Huyo Ataingia Peponi

 

Itaendelea In Shaa Allah….

 

Mwandishi: Sheikh Abu Hanifa Salim Mwinyi, Allah Amuhifadhi.

Mchapishaji: salafussaalih.net

Tarehe: 11 Rabiu al-Thaaniy 1447H

 

Rejea:

1. Qur’aan Suratul Layl:17

2. Sahih Muslim.