2. Ubora Wa Maswahaba Allah Awaridhie
فضل الصحابة رضي الله عنهم
Hakika Fadhla Za Maswahaba Ni Nyingi Mno Na Ubora Wao Haufananishwi Na Mwanadamu Yeyote Baada Ya Mitume Wa Allah.
Maswahaba Walikuwa Wakali Kwa Makafiri, Pia Walikuwa Wakihurumiana Wao Kwa Wao
قال الله تعالى:
[مُّحَمَّدٞ رَّسُولُ ٱللَّهِۚ وَٱلَّذِينَ مَعَهُۥٓ أَشِدَّآءُ عَلَى ٱلۡكُفَّارِ رُحَمَآءُ بَيۡنَهُمۡۖ تَرَىٰهُمۡ رُكَّعٗا سُجَّدٗا يَبۡتَغُونَ فَضۡلٗا مِّنَ ٱللَّهِ وَرِضۡوَٰنٗاۖ]
Amesema Mola Aliyetukuka:
” Muhammad Ni Mtume Wa Allah Na Wale Waliopamoja Naye Ni Wakali Kwa Makafiri Na Niwenye Kuhurumiana Wao Kwa Wao Utawaona Wakirukuu Na Kusujudi Kwa Pamoja Wakitafuta Fadhla Kutoka Kwa Allah Na Radhi Zake.” [Surat al-Fath:29]
Muumini Bora Ni Yule Ambaye Huguswa Na Jambo La Muumini Mwenzake, Na Hivi Ndivyo Walivyokuwa Maswaha.
Tujiangalie Sisi Katika Miamala Yetu Na Mafungamano Yetu Tupoje…!?
Imesimuliwa Hadithi Kutoka Kwa Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake.
عن نعمان ابن بشير رضي الله عنه قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: مثل المؤمنين في توادهم وتراحمهم وتعاطفهم كمثل الجسد إذا اشتكي منه عضوا تداعى له سائر الجسد بالسهر والحمى
Kutoka Kwa Nu’maan Ibu Bashir Radhi Za Allah Ziwe Juu Yake Amesema: Amesema Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake: “Mfano Wa Waumini Katika Kupendana Kwao Na Kuoneana Kwao Huruma Ni Kama Mfano Wa Kiwiliwili, Pindi Kitakapopata Shida Kiungo Kimoja Uenea Maumivu Mwili Mzima Kwa Kukesha Na Homa (Kuumwa)”
2. Baadhi Ya Sifa Za Maswahaba
- Ni Wenye Huruma Sana.
- Ni Weledi Mno Kwenye Masuala Ya Dini.
- Ni Wenye Pupa Mno Katika Mambo Ya Kheri Na Wenye Mapenzi Mno Na Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake.
Maswahaba Ni Watu Wanaofaa Kufuatwa Na Kuigwa Mwenendo Wao.
Amesema Ibnu Masuud Allah Amridhie:
Atakayekuwa Miongoni Mwenu Ni Mwenye Kufuata Basi Na Awafuate Maswahaba Wa Mtume Muhammad Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake, Kwa Sababu Maswahaba Wananyoyo Safi Na Niweledi Mno Katika Mambo Ya Dini.
Itaendelea In Shaa Allah….
Mwandishi: Sheikh Abu Hanifa Salim Mwinyi, Allah Amuhifadhi.
Mchapishaji: salafussaalih.net
Tarehe: 30 Rabiu al-Awwal 1447H
Rejea:
1. Qur’aan Suratul Fath:29
2. Bukhar Na Muslim
3. Jaamiul Bayaan Al’ilm Wafadhlihi 2/942