1. Ubora Wa Maswahaba Allah Awaridhie
فضل الصحابة رضي الله عنهم
Alhamdulillahi Waswalatu Wasalaam Ala Rasuuli Llaahi
Ammaa Baad:
Baada Ya Kumuhimidi Allah Aliyetukuka Na Kumtakia Swala Na Salaam Kiongozi Wetu Wa Ummah Mtume Wetu Muhammad Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake.
Katika Kufahamu Ubora Wa Maswahaba Tumeona Ipo Haja Kubwa Kuangalia Taarifu Za Wanazuoni Wetu Juu Ya Kumtambua Ni Nani Swahaba.
1.Taarif Ya Swahaba
Amesema Al-Imam Ibnu Hajar Al-Asqalany Allah Amraham:
Neno Swahaba Kilugha Lina Maana Mwenye Kulazimiana Na Kitu, (Au Jambo Au Mtu).
Swahaba Ni Yule Aliyekutana Na Mtume Hali Ya Kuwa Amemuamini Na Akafa Hali Ya Kuwa Na Iman, Ata Kama Atapitikiwa Na Kurtad.
Na Kwa Taarif Hii Ambayo Ameitaja Ibnu Hajar Al-Asqalany Hatozingatiwa Mtu Kuwa Ni Swahaba Kama Hajakutana Na Mtume Hata Kama Alikuwa Katika Zama Za Mtume, Kwa Mfano Najash Hakumuona Mtume Na Alipokufa, Mtume Akamswalia Najash Akiwa Katika Mji Wao Habash.
Miongoni Mwa Mifano Mizuri Ni Taabiiyu Al-Jaliil Abuu Idrisa Al-Khawalaany, Huyu Alifika Katika Mji Wa Madina Hali Ya Kuwa Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake Ameshakufa Kwa Siku Moja Au Mbili Kabla, Hivyo Si Katika Maswahaba Kama Walivyotaja Ahalul Ilmi.
Imam Ahmad Ibnu Hanbal Allah Amraham Amesema:
Swahaba Ni Kila Aliyesuhubiana Na Mtume Mwaka Mmoja Au Mwezi Au Siku Au Saa Na Akamuona Mtume Naye Atakuwa Ni Swahaba Wake Kwa Qadri Alivyosuhubiana Na Mtume.
Hakuna Shaka Kuwa Wanapotajwa Maswahaba Huwa Wanakusudiwa Muhajirina Na Answar.
Amesema Allah Aliyetukuka Katika Surat at-Tawbah:
[وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلۡأَوَّلُونَ مِنَ ٱلۡمُهَٰجِرِينَ وَٱلۡأَنصَارِ وَٱلَّذِينَ ٱتَّبَعُوهُم بِإِحۡسَٰنٖ رَّضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُ وَأَعَدَّ لَهُمۡ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي تَحۡتَهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ]
Na Wale Waliotangulia Wa Mwanzo Miongoni Mwa Muhajirina Na Answar Na Wale Watakaowafuata Hao Kwa Wema Allah Awaridhie Nao Wamridhie Allah Na Mola Amewahaidi Pepo Ipitayo Chini Yake Mito Wataishi Humo Milele Huko Ndiko Kufaulu Kuliko Kukubwa. [Surat at-Tawbah:100]
Ametaja Al-Imam Twabary Allah Amraham Katika Kutafsir Aya Iliyotangilia Hapo Juu:
A. Waliotangulia Wa Mwanzo:
Waliowatangulia Watu Kumuamini Allah Na Kumuamini Mtume Wake.
B. Al-Muhajiruun:
Ni Wale Ambao Waliwahama Watu Wao Na Jamaa Zao Na Wakaacha Majumba Yao Na Miji Yao.
Taaliq: Mfano Wa Watu Walioacha Miji Yao Ni Abuubakri Swiddiiq, Abdulrahmaan Ibnu Awfy Na Wengineo.
C. Wal-Answar :
Na Answar Ni Wale Waliomnusuru Mtume Swala Na Salaam Ziwe Juu Yake Juu Ya Maadui Zake Miongoni Mwa Makafiri.
Itaendelea In Shaa Allah….
Mwandishi: Sheikh Abu Hanifa Salim Mwinyi, Allah Amuhifadhi.
Mchapishaji: salafussaalih.net
Tarehe: 25 Rabiu al-Awwal 1447H
Rejea:
1. Qur’aan at-Tawbah:100.
2. Tafsiri Twabar
3. Nuzhatul Fikar
4. Musnal Imam Ahmad